Radio Osotua › Local News

KUCCPS Yatoa Matokeo Ya Uteuzi Wa Vyuo Vikuu.

Local News July 8, 2026 Brigit Agwenge

Zaidi ya wanafunzi laki moja walioandika mtihani wa KCSE mwaka uliopita walituma maombi ya kujiunga na vyuo vikuu na taasisi za Anuwai kupitia tovuti ya KUCCPS.

Akitangaza matokeo ya uteuzi wa wanafunzi wa vyuo vikuu wa mwaka 2026/2027, Waziri wa Elimu Julius Ogamba amesema kuwa jumla ya wanafunzi 293,869 wameteuliwa katika programu za shahada, stashahada na kozi za kiufundi.

Vilevile kati ya idadi hiyo, kuna wale ambao wameteuliwa kujiunga na taasisi ya mafunzo ya matabibu KMTC huku wengine wakitarajiwa kujiunga na taasisi za mafunzo ya walimu TTC.

Aidha wanafunzi wengine 8,915 waliofuzu kwa program ya shahada, walituma maombi ya kujiunga na vyuo vya Anuwai. Kando nahayo, KUCCPS imesema kuwa kozi ya Shahada ya Tiba ilikuwa na ushindani mkubwa katika nafasi za 2026/2027.

Afisa Mkuu Mtendaji wa KUCCPS Agnes Wahome alibainisha kuwa kati ya wanafunzi 6500 waliotuma maombi ya kosi ya udaktari, kulikuwa na nafasi kwa wanafunzi 702 pekee katika vyuo vikuu vyote vya umma na vya kibinafsi nchini Kenya, na kufanya mchakato huo kuwa wa ushindani mkubwa.