Radio Osotua › Local News

Serikali ya kaunti ya Kisii kusambaza matenki ya maji mashuleni

Local News August 4, 2023 Osotua

BY ISAYA BURUGU 4TH AUG 2023-Serikali ya kaunti ya Kisii imeanza mpango wa kusambaza matenki ya maji   katika shule  zinazokumbwa na changamoto za kupata maji.

Vilevile mpango huo unaohusisha wizara ya maji ya kaunti hiyo unanuiwa kukabili magonjwa yanayoletwa na matumizi ya maji chafu kama vile kipindupindu.

Mpango huo uliyoanzishwa na gavana Simba Arati unalengo shule moja kati ya wadi 45 katika kaunti ya Kisii.

.