Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki nchini (KCCB) limelaani vikali mauaji ya mapadre wawili yaliyotokea ndani ya kipindi cha juma moja, likiitaka serikali kuhakikisha haki inatendeka.
Kupitia Idara ya Haki na Amani (CJPD), KCCB imeeleza masikitiko yake kutokana na mauaji ya Padre John Maina Ndegwa na Padre Allois Cheruiyot Bett, na kuyataja kama vitendo vya ukatili visivyokubalika katika jamii yoyote inayojali utu wa binadamu.
Katika taarifa hiyo iliyotolewa Alhamisi usiku, baraza hilo limehimiza vyombo vya usalama kufanya uchunguzi wa kina na kuhakikisha kwamba usalama unapatikana kwa wananchi na kutokomeza mauaji ya kiholela.
🕊️ We mourn Fr. John Maina Ndegwa and Fr. Allois Cheruiyot Bett, both violently killed within a week. Their deaths are a tragic loss to the Church and nation. We call for urgent govt action to ensure justice, safety, and an end to impunity.#JusticeAndPeace #CJPD #Kenya
— KCCB – Catholic Justice & Peace Department (@CJPDKENYA) May 22, 2025
Taarifa ya polisi iliyotolewa siku hiyo hiyo imeeleza kuwa watu sita wamekamatwa kuhusiana na mauaji ya Padre Cheruiyot Bett, ambaye alikuwa akihudumu katika Parokia ya Mtakatifu Matthias Mulumba Tot. Padre huyo aliuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana katika kijiji cha Kabartile, Kaunti ya Elgeyo Marakwet.
PRESS STATEMENT : SHOOTING INCIDENT INVOLVING FATHER ALLOIS BETT pic.twitter.com/MneTAN4wM4
— National Police Service-Kenya (@NPSOfficial_KE) May 22, 2025
Polisi wamesisitiza kuwa uchunguzi unaendelea na juhudi zaidi zinafanywa ili kuwakamata washukiwa wengine. Aidha, wamelipinga dai kuwa mauaji hayo yanahusiana na visa vya wizi wa mifugo vilivyoshuhudiwa katika maeneo ya kaunti hiyo.