OGOLLA

Mkuu wa Majeshi Jenerali Francis Ogolla Kuzikwa Siku ya Jumapili Familia Yasema.

Aliyekuwa Mkuu wa majeshi humu nchini Marehemu Jenerali Francis Ogolla, ambaye alifariki katika ajali ya ndege katika kaunti ya Elgeiyo Marakwet, atazikwa Jumapili ya tarehe 21 mwezi wa Aprili nyumbani kwake katika eneo la Alego Usonga, Kaunti ya Siaya. Kulingana na taarifa…

Askofu mkuu Maurice Muhatia ateuliwa kuwa mwenyekiti wa Baraza la maaskofu KCCB.

Askofu mkuu wa jimbo kuu la Kisumu Maurice Muhatia Makumba ameteuliwa kuwa mwenyekiti wa baraza la maaskofu wa kanisa katoliki KCCB kwa muda wa miaka tatu ijayo. Askofu mkuu Muhatia, anachukua nafasi hii kutoka kwa Askofu mkuu wa jimbo kuu la Mombasa…

KUTRRH

Hospitali ya KUTRRH Yaajiri Madaktari Wa Kigeni Kuwatibu Wagonjwa wa Saratani.

Hospitali ya Rufaa, Mafunzo na Utafiti ya Chuo Kikuu cha Kenyatta (KUTRRH) imetangaza hatua ya kuwaajiri madaktari watano wa kigeni ili kuongeza uwezo wa kutoa huduma bora za matibabu kwa wagonjwa. Hatua hii inakuja wakati ambapo matabibu nchini wanashiriki mgomo, ambao umeingia…

Maandamano ya Madaktari

Madaktari Kushiriki Maandamano ya Amani Jumanne kushinikiza Utekelezaji wa CBA

Muungano wa Madaktari nchini, KMPDU, umetangaza mipango ya kuandaa maandamano ya amani siku ya Jumanne ijayo, lengo likiwa ni kuendelea kuisukuma serikali kusikiliza kilio chao. Katibu Mkuu wa KMPDU, Davji Atellah, kupitia barua aliyoituma kwa Kamanda wa Polisi wa Kaunti ya Nairobi,…

Mgomo wa madaktari waingia siku ya 22 leo hii.

Muungano wa madaktari nchini KMPDU umeendelea kumkashifu waziri wa afya Susan Nakuhmicha kwa kupendekeza kupunguzwa kwa mishahara ya madaktari wanagenzi kinyume na ilivyoainishwa kwenye mkataba wa maelewano wa mwaka 2017. Wakiwahutubia waandishi wa habari jijini Nairobi,muungano huo umeeleza kuwa mshahara ambao wanagenzi…

Ghana - Kenya

Ghana Kuunga Mkono Azma ya Raila Odinga Kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika.

Serikali ya taifa la Ghana imeahidi kuunga mkono azma ya Kinara wa chama cha ODM Raila Odinga, ya kuwania wadhifa wa mwenyekiti wa Muungano wa Umoja wa Afrika (AU). Rais William Ruto, ambaye yupo katika ziara rasmi nchini Ghana, aliweka wazi taarifa…

Ajali - Salama Area

Watu 10 Waangamia Kwenye Ajali ya Magari 5 Kwenye Barabara ya Nairobi- Mombasa.

Watu kumi wamepoteza maisha yao huku wengine kumi na wawili wakijeruhiwa vibaya katika ajali mbaya ya barabarani iliyohusisha magari kadhaa, ikiwemo matatau na Trella, katika eneo la Salama kwenye barabara kuu ya Nairobi – Mombasa. Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa asasi…

Rev, John Kiplimo

Jimbo la Eldoret Lapata Askofu Mpya Msaidizi baada ya Uteuzi wa Papa Francis Leo

Jimbo Katoliki la Eldoret limepokea habari njema baada ya Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis, kumteua Padre John Kiplimo Lelei kuwa Askofu Msaidizi. Kabla ya uteuzi huu, Padre Lelei alikuwa akihudumu kama Vicar Generali wa Jimbo hilo la Eldoret. Taarifa rasmi…