BY ISAYA BURUGU 16TH JAN 2022-Maafisa wa polisi wametakiwa kushirikiana na kanisa ili kama njia moja ya kutatua changamoto zinazoambatana na misongo ya mawazo wakiwa kazini.

Akizungumza baada ya kushiriki misa maalum na ufunguzi wa kanisa ndani makazi ya polisi wa mji wa Narok Kamishna wa Kaunti ya Narok Isaac Masinde alisisitiza haja ya maafisa hao kushiriki maombi katika kanisa hilo.Masinde aliwashukuru maafisa hao kwa kushiriana na idara zingine kufanikisha uchaguzi pamoja na mitihani ya kitaifa kama ipasavyo hasa katika kaunti ambayo inajumuisha makabila mengi ili kufaulisha ajenda ya Rais William Ruto.

 Padri Edmond Tarimo Kiringosi wa Parokia ya Mtakatifu Petro Narok mjini aliyeongoza sherehe hiyo kwa upande wake akiunga semi za Masinde aliyejuta jinsi baadhi ya maafisa wamejitoa uhai.Kiringosi akiwarai tenga muda wakushiriki maombi kwani jimbo hilo sasa limepata katekisti ambaye atawaelekeza kiroho.I

wiki jana ambapo Rais Ruto alishudia kufuzu kwa askari wa polisi ambapo aliahidi kushughulikia maslahi yao.

 

January 16, 2023