Radio Osotua › Local News

Bei ya Mafuta nchini kusalia sawa na ya mwezi Disemba 2022 – EPRA

Local News January 14, 2023 John Waicua

Bei ya mafuta nchini haitabadilika kw akuongezeka au kupungua katika kipindi cha mwezi mmoja ujao. Taarifa kutoka kwa mamlaka ya udhibiti wa Nishati nchini imesema kuwa mafuta ya Super Petrol yataendelea kuuzwa kwa shilingi 177 kwa lita, Dizeli ikiuzwa kwa shilingi 162 kwa lita, na Mafuta ya Taa kwa shilingi 145.9 kwa lita, bei sawa na ile ambayo mafuta haya yalikua yakiuzwa mwezi Desemba mwaka jana.