Karibia miezi miwili baada ya gavana wa Narok Patrick Ntutu kuahidi kuwa kampuni ya umeme ya Kenya power tawi la Narok, itatatua tatizo la ukosefu wa taa za barabarani, baadhi ya wakaazi wa Narok mjini wameibua malalamishi wakisema kuwa taa hizo bado hazijaweza kushugulikiwa.
For some time now, streetlights in Narok Town and other urban centres across the county have been non-functional, posing a security risk and hindering evening business operations.
This morning, I held a meeting at my office with officials from Kenya Power, during which we… pic.twitter.com/QWwUvjnYMl
— Governor Patrick Ole Ntutu (@OleNtutuK) July 22, 2025
Kulingana na wakaazi hao ambao wamezungumza na kituo hiki cha Radio Osotua, ukosefu wa taa hizo umeathiri pakubwa biashara zao hasa majira ya usiku ikizingatiwa kuwa wanalazimika kufunga biashara zao mapema, wakihofia usalama wao kutokana na giza.