Aliyekuwa naibu wa rais Rigathi Gachagua hii leo amezuru mji wa Narok ambapo amewahutubia wananchi katika eneo la rungu ya Moi.
Gachagua aliandamana na viongozi mbalimbali akiwemo kinara wa wiper Kalonzo Musyoka, Kinara wa PLP Martha Karua, Eugene wamalwa wa DAP-K pamoja na aliyekuwa mwanasheria mkuu Justin Muturi.
Kiongozi huyo wa DCP, ameendeleza kampeni zake dhidi ya utawala wa Kenya Kwanza akidai kuwa mkuu wa nchi rais William Ruto amenyakua mashamba mengi katika kaunti ya Narok.
A sea of humanity in one collective has spoken from Narok on an unstoppable liberation cause of our country Kenya.
We have heard your cry like all other Kenyans.
There is great hope and light ahead that our nation will be free again; there will be no abductions and anarchy, no… pic.twitter.com/AevxQ76f6i
— Rigathi Gachagua (@rigathi) June 30, 2025
Kwa upande wa viongozi walioandamana na Gachagua, wamekashifu vikali visa vya vijana kukamatwa kiholela na wengine hata kutoweka.
Narok na Kenya mzima wameamua Ruto ni #WanTam! pic.twitter.com/QJEraqeSIN
— Kalonzo Musyoka (@skmusyoka) June 30, 2025