Chama tawala cha UDA kimetangaza ubabe wake kwa mara nyingine baada ya wagombea wake kushinda katika maeneo 3 kati ya 4 yaliyoandaa uchaguzi mdogo hio jana.
Katika kaunti ya Murang’a Chege njuguna sasa ndiye mbunge mpya mteule wa eneobunge la Kandara, baada yake kuibuka mshindi katika uchaguzi mgogo wa ubunge ulioandaliwa hio jana. Njuguna ambaye alikuwa mwaniaji wa chama cha UDA, alijizolea kura 21,650 na kumpiku mpinzani wake wa karibu Titus Njau wa chama cha Ford Asili aliyejizolea kura 14,678.
Uchaguzi huo ulifuatia uteuzi wa aliyekuwa mbunge wa eneobunge Hilo Alice Wahome katika baraza la mawaziri. Njuguna atachukua mikoba ya kuliongoza eneo hilo kama mbunge baada ya kuapishwa kwake katika bunge la kitaifa.