30TH DEC,2023-Gavana wa Trans Nzoia George Natembeya amependekeza mpango mpya ambapo wakazi watachangia gunia moja la kilo 90 za mahindi kila mwaka ili kujiandikisha katika Hazina ya Kitaifa ya Bima ya Afya (NHIF).

Akihutubia wakazi katika kambi ya matibabu ya bure huko Namanjala, Gavana huyo alibainisha kuwa pendekezo hilo linalenga kuwaondolea wakazi changamoto kubwa za kifedha za kupata huduma za afya bila bima ya matibabu.

Pendekezo la Gavana Natembeya linafuatia wito wake wa hivi majuzi kwa waendesha bodaboda kujiandikisha katika huduma ya NHIF kama sehemu ya mpango ambao unaweza kupanua huduma za afya kwa wakazi wote katika kaunti hiyo.

Gavana Natembeya pia aliwahimiza wakazi kutumia kwa makini vituo vya afya vilivyo karibu, akisisitiza umuhimu wa kuchunguzwa mara kwa mara ili kugundua magonjwa mapema.Hii, alibainisha, itawawezesha kutekeleza mara moja hatua za kuzuia.

 

December 30, 2023