Chama cha Wanasheria nchini (LSK) kimelaani ukatili wa polisi na madai ya kushirikiana na makundi ya raia wenye silaha wakati wa maandamano ya jana.

    Maandamano hayo jijini Nairobi yalisababisha majeraha kwa watu 17, akiwemo mchuuzi aliyepigwa risasi kwa karibu na afisa wa polisi.

    LSK ilikosoa vikali mwenendo wa vikosi vya usalama katika taarifa yake, ikitoa ushahidi wa kutumia nguvu kupita kiasi dhidi ya waandamanaji.

    Kulingana na chama hicho, makundi hayo ya wahuni, yaliwanyanyasa na kuwatisha raia, hivyo kuibua wasiwasi mkubwa kuhusu ukiukwaji wa haki za binadamu na kuvunjika kwa utawala wa sheria.

    June 18, 2025

    Leave a Comment