BY ISAYA BURUGU  ,1ST DEC 2022-Kenya inaungana na ulimwengu leo  kuadhimisha siku ya  ukimwi duniani  huku maambukizi ya virusi vya HIV na ugonjwa wa Ukimwi yakiripotiwa kuongezeka kwa mara ya kwanza nchini katika muda wa miaka kumi iliyopita.Haya ni kwa mjibu wa ripoti.

Ripoti hiyo ya maadhimisho ya siku ya ugonjwa wa Ukimwi  duniani mwaka   itakayozinduliwa leo  inadokeza kuwa Kenya  ilirekodi  ongezeko  la maambukizi mapaya  ya HIV  kwa mara ya akwanza ndani ya miaka kumi  kwa  Zaidi ya visa 2000  kutoka  visa alfu  32,025  hadi kufikia visa 34, 540.

Katika kipindi cha mwaka jana pekee Kenya ilisajili visa vipya vya maambukizi ya HIV vipatavyo 34,540 HIV .

Ripoti hiyo inahusisha hali hiyo  na maambukizi mapaya miongoni mwa Watoto ,vijana wanaobalehe na watu wachanga  sawa  na upungufu  wa dawa za kukabili makali ya ugonjwa wa Ukimwi.

Ripoti hiyo kwa jina it is a race against time iliyoandaliwa na baraza la kitaifa la  kudhibiti magonjwa yaani the  National Syndemic Disease Control Council imefichua kuwa  visa vipya vya maambukizi ya virusi vya HIV Vipatavyo  34,540  vilisajiliwa huku   asilimia  70  kati ya visa hivyo  jumla ya 20,505 vikisajiliwa  miongoni mwa wanawake na wasichana .

 

December 1, 2022