Radio Osotua › Local News

Matayarisho ya mitihani ya KCPE na KPSEA yandaliwa nchini huku mtihani huo ukitarajiwa kuanza jumatatu ijayo

Local News October 27, 2023 Osotua

BY ISAYA BURUGU,27TH OCT 2023-Zoezi la mwigo kwa minajili ya mtihani  wa kitaiafa kwa darasa la nane KCPE na tathmini ya KPSEA  inayotarajiwa kuanza jumatatu wiki ijayo limefanyika katika shule mbali mbali nchini leo.

Wanafunzi milioni 1.4 watafanya KCPE katika vituo 28,533 kote nchini. Wanafunzi milioni 1.28 nao watafanya tathimini ya KPSEA katika vituo 32,584.

Katika shule ya msingi ya Roots kaunti ya Nakuru hali ya imekuwa shwari huku zoezi hilo la mwisgo likiendeshwa vyema.Mwalimu mkuu wa shule hiyo Colins Odhiambo ameelezea  Imani kuwa mandalizi waliofanya yatawapa matokeo bora.

 Watainiwa wa KCPE mwaka huu ndio wa mwisho kabla ya mtaala wa elimu wa 8-4-4 kutamatika rasmi.