BY ISAYA BURUGU  13TH  JAN 2023-Mwili wa mwalimu wa miaka 44 aliyeripotiwa kupotea  tarehe 22 mwezi disemba mwaka jana umepatikana ndani ay sanduku  nyumbani mwake katika Kijiji cha  Ihururu kaunti ya Nyeri.

Mabaki ya Joseph Gathogo yamepatikana  ndani ya chumba chake cha  sebule baada ya harufu mbaya kuanz akutoka  katika nyumba hiyo na kupelekea msimamizi wa nyumba Wiliam Gitau kuwapasha polisi Habari ambao walivunja nyumba ya marehemu.

Waligundua  mwili wa mwalimu huyo wa shule ya sekondari ya Muhoya ukiwa umegongelewa misumari  kwenye sanduku lililokuwa na muundo wa mashua lililokuwa kama kaburi.Shada la maua ,bendera nyeusi na mandishi yasiyosomeka yalipatikana na pembe  vilipatikana kando ya mwili huo.

Kwa mjibu wa naibu chifu wa  Muhoya Martha  Wanjiru  amesema siku ya kutoiweka kwake Mwlaimu huyo alikuwa ametoka kusimamia mtihani wa kidato cha nne KCSE uliyokuwa ukiendelea.Na hakuonekana tangu wakati huo.

 

 

 

 

January 13, 2023