Mwili wa Papa Francis ulihamishwa asubuhi ya leo kutoka Kanisa la Casa Santa Marta hadi Kanisa Kuu la St. Peter’s Basilica mjini Vatican, ambako waumini kutoka sehemu mbalimbali watapata fursa ya kutoa heshima zao za mwisho.
Mwili huo utasalia ndani ya basilika hiyo kwa muda wa siku tatu, na waumini wataruhusiwa kuendelea kumuaga kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki aliyeaga dunia Jumatatu, Aprili 21.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Vatican, ibada rasmi ya mazishi itaandaliwa siku ya Jumamosi, ikiongozwa na Kardinali Giovanni Battista Re, Mkuu wa Chuo cha Makardinali.
Baada ya misa ya mazishi, mwili wa Papa Francis utaelekezwa katika Kanisa Kuu la St. Mary Major Basilica, ambako utazikwa siku hiyohiyo ya Jumamosi.
The mortal remains of Pope Francis are carried up the steps of St. Peter’s Basilica and into the Vatican Basilica.
The Rite of Translation from the Casa Santa Marta was led by members of the College of Cardinals present in Rome, and over 20,000 people gathered in the square to… pic.twitter.com/c2GTXjVBrW
— Vatican News (@VaticanNews) April 23, 2025
The mortal remains of Pope Francis have been transferred from the Casa Santa Marta to St. Peter’s Basilica, where his body will lie in state so the faithful may pay their respects until his funeral on Saturday.https://t.co/FyrPEWWuET
— Vatican News (@VaticanNews) April 23, 2025