Hussein Mohammed

Rais William Ruto amefanya uteuzi wa maafisa 10 wapya katika Afisi Kuu ya Rais Ijumaa 14.10.2022. Katika orodha ya uteuzi huo, Rais amemteua aliyekuwa mwanahabari wa Runinga ya Citizen Hussein Mohammed kama msemaji wa Ikulu huku mwanauchumi David Ndii akiteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la washauri wa Rais kuhusu maswala ya Kiuchumi. Orodha kamili ya watu walioteuliwa inajumuisha

Felix K. Koskei – Mkuu wa Wafanyakazi na Mkuu wa Utumishi wa Umma

Aliyekuwa gavana wa Turkana Josphat Nanok – Naibu Mkuu wa Wafanyakazi

Dkt. Augustine Cheruiyot – Mshauri Mkuu & Mkuu wa Sekretarieti ya Mabadiliko ya Kiuchumi

Dkt. Kamau Thugge – Mshauri Mkuu na Mkuu wa Masuala ya Fedha na Sera ya Bajeti

Mohammed Hassan na Nancy Laibuni – Mjumbe, na Mjumbe mshirikishi wa Baraza la washauri wa rais katika maswala ya Kiuchumi

Katoo Ole Metito – Mdhibiti wa Ikulu

Bw. David Mugonyi – Mkuu wa Huduma ya Mawasiliano ya Rais

October 14, 2022