Radio Osotua › Local News

Bunge la kaunti ya Narok lapitisha bajeti ya shilingi billioni 15.4.

Local News December 6, 2022 Brigit Agwenge

Bunge la kaunti ya Narok limepitisha bajeti ya shilingi billioni 15.4. Kulingana na mwenyekiti wa bajeti Timothy Ole Maku na ambaye pia ni mwakilishi wadi wa Naikara ni kwamba kila sekta itapokea mgao kutoka kwa bajeti hiyo.

Kwa upande wake kiongozi wa walio wengi bungeni Songoi Lemein amewashukuru wawakilishi wadi kwa kupitisha bajeti hiyo na kutoa hakikisho kuwa watashirikiana ili kufanya maendeleo katika kaunti hii.