BY ISAYA BURUGU 27TH DEC 2022-Mkurugenzi mkuu wa mashataka ya umma Noordin Haji amewasilisha rufaa mahakamani akipinga hatua ya hakimu mkuu Douglas Ogoti  kumwachilia aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Mbuvi  Sonko katika kesi ya ufisadi wa shilingi milioni 20 iliyokuwa ikimwandama.

Hakimu Ogoti mnamo deseimba tarehe 21  alitupilia mbali kesi  dhidi ya SONKO  na mtuhumiwa mwenzake Antony Ombok .Wawili hao walikuwa wanakumbwa na mshatak 13 yanayohusiana na kesi hiyo.

Hakimu Ogot alitaja ukosefu wa ushahidi kama sababu yah atua yake.DPP Haji hata hivyo  anasema hakimu Ogot katika kutoa uamuzi huo  alitegemea stakabadhi za zamani  zilizowasilishwa tarehe 27 Januari mwaka 20202 na kupuuza zile zilizowasilishwa tarehe 7 septemba mwaka huo ambazo anasema ndizo zilizoelezea uzito kwa kesi hiyo.

Kwa mjibu wa Haji Hakimu Ogot alikosea  kisheria  alipotangaza kuwa mashataka hayo yalikuwa na kasoro  licha yake kukubali stakabadhi mpya zilziofanyiwa marekebisho kuhusu kesi hiyo.

Sasa Haji anataka mahakama ya rufaa kutupilia mbali uamuzi huo wa hakimu Ogoti na kuagiza SONKO na wenzake kujitetea mahakamani.

 

December 27, 2022