BY ISAYA BURUGU,10TH FEB,2023-Hazina ya kitaifa ya malipo ya uzeeni NSSF sasa inawataka waajiri kuheshimu mara moja agizo la mahakama linalowataka  kuongeza kiwango cha fedha wanazowatoza wafanyikazi wao  kuelekea kwenye hazina hiyo kila mwezi.

Kupitia taarifa  iliyotolewa leo mwenyekiti wa hazina hiyo Antony Munyiri  waajiri wamekuwa wakitimiza   sheria nambari 45 ya mwaka 2013 na wanapasw akuendelea kufanya hivyo huku  akiwataka wasiofanya hivyo kuanza kufanya hivyo mara moja

.Ada hizo mpya zitapelekea  mwajiri na mfanyikazi wake wakichangia shilingi 2160 kutoka kiwango cha sasa cha shilingi mia mbili.Kwa mjibu wa NSSF kila mwajiri atahitajika kulipa ada hizo mpya kufikia tarehe tisa kila mwezi.

Haya yanajiri baada ya majaji watatu wa mahakama ya rufaa, Hannah Okwengu, Mohamed Warsame naJohn Mativo  kubatiliza   agizo lililotolewa na mahakama kuu mnamo septemba mwaka jana  lililokuwa limetangaza sheria ya NSSF yam waka 2013 kuwa kinyume cha katiba,kwani wananchi hawakuhusishwa .

 

 

 

February 10, 2023