BY ISAYA BURUGU 22ND NOV 2022-Serikali ya kaunti ya Kisumu imezindua  mkakati wa utoaji huduma msingi za kiafya  unaotilia maanani  kuzuia magonjwa  huku washirika  wakiitisha kutengewa fedha Zaidi za mpango huo.Mpango huo wa miaka miwili  unatokana na na mpango wa kitaiafa wa uboreshwjai wa afysy msningi wa kati yam waka  2019-2024.

Dakita  Kennedy Otieno, ambaye ni naibu kurugenzi mkuu wa huduma za kiafya kwenye kaunti hiyo  amesema kuwa asilimia 80 ya magonjwa yanaweza kukabiliwa kikamilifu kwenye kiwnago cha nyumba .Otieno amesema hospitali zitaendelea kutoa huduma zake za kuponya  lakini magonjwa mengi  yanaweza shughulikiwa nyumbani .

Mmmoja wawashiriki wakuu katika kubuni mkakati huo Patricia Orao, ambaye ni mkurugenzi mkuu wa  shirika la stawisha Dada  amesemaa afya bora inapaswa kuwa  jukumu na shabaha ya   kila mkenya.

Akizungumza na wandishi Habari wakati wa uzinduzi wa mpango huo jijini Kisumu Oraro amesema mkakati huo unalenga kuhakikisha kuwa kila mtu katika kiwango cha familia  anachukua udhibiti wa Maisha yao ili kujiepusha na matumizi ya kiwango cha juu cha kifedha kusaka matibbau.

 

November 22, 2022