Mwanaume mmoja wa umri wa makamo ametiwa mbaroni katika msitu wa Loita eneobunge la Narok kusini akihusishwa na hulka ya ukataji wa miti na uharibifu wa misitu. Akidhibitisha haya, naibu kamishana wa kaunti ndogo ya Narok kusini Bw. Felix Kisalu amesema mwanaume huyo aliyetambuliwa kama Wilson Keuwa, amekuwa mafichoni kwa wiki moja baada ya taarifa kuwa anawindwa na maafisa wa polisi.