BY ISAYA BURUGU,23RD FEB,2023-Maafisa wa polisi kaunti ya  Homa Bay  wanamzuilia  mwanamke wa miaka 23 anayetuhumiwa  kumu ana kutupa mwili wa mtoto wake mchanga  baada ya kumzaa nyumbani mwake katika mtaa wa Makongeni  mjini Homa Bay.

Mwanamke  huyo alikamatwa baada ya wakaazi wa Makongeni kuupata mwili wa mtoto huyo kakatika jaa la kutupa taka.

Kwa mjibu wa naibu chifu wa  lokesheni ndogo ya Simenya  Erick Odhiambo, mshukiwa alikamatwa na polisi  baada ya kundi la wanawake  na afisi yake kuendesha msako  wa mwanamke yeyote ambaye amezaa na kumtupa mwanawe  ndipo walipompata mwanamke huyo.

Amesema mshukiwa aliwadhibitishia polisi kuwa yeye ndiye aliyekuwa amemua na kutupa mwili wa mtoto huyo hata ingawa hakutoa sababu za kitendo hicho.

Kamanda wa polisi kaunti ya Homa-Bay  Samson Ole Kinne amedhibitisha kukamatwa kwa mwanamke huyo ambaye anazuiliwa akisubiri kufikishwa mahakamani.

 

February 23, 2023