Radio Osotua › Local News

Tume ya kitaifa ya polisi kuwahoji waliotuma maombi kwa wadhifa wa mkurugenzi wa DCI

Local News October 11, 2022 Osotua

By  Isaya Burugu,Oct 11,2022-Tume ya kitaifa ya huduma kwa polisi hivi leo inawahoji waliotuma maombi kujaza nafasi ya mkurugenzi mkuu wa idara ya upelelezi wa jinai DCI.

Hatua hiyo inafuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa mkurugenzi George Kinoti.Watu kumi wametuma maombi ya kujaza nafasi hiyo.

Mahoijiano hayo yanandaliwa katika chuo cha mafunzo ya serikali yaani Kenya school of government jijini Nairobi.