Tume ya Utumishi wa Umma (PSC) imetoa mwaliko kwa wananchi wenye nia ya kuwania nafasi ya makatibu waratibu katika wizara mbalimbali (CAS) kutuma maombi yao ya nafasi hizi kabla ya Oktoba 27. Katika taarifa iliyochapishwa Jumatano 12.10.2022 na mwenyekiti wa PSC Anthony Muchiri, wanawake, watu kutokaa jamii za walio wachache pamoja na walemavu wamehimizwa kuchuua nafasi hii kutuma maombi yao ya kazi hizi.