Radio Osotua › Local News

Aliyekuwa mbunge wa malindi Aisha Jumwa apata afueni baada ya ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma kuondoa kesi ya ufisadi dhidi yake.

Local News October 12, 2022 Brigit Agwenge

Waziri mteule wa masuala ya Jinsia Aisha Jumwa amepata afueni baada ya afisi ya mkurugenzi wa mashataka ya umma kuondoa kesi ya ufisadi dhidi yake.

Jumwa alikuwa akikabiliwa na kesi ya ufisadi ya shilingi milioni kumi na tisa,pesa anazodaiwa kuziiba kutoka kwa hazina ya maendeleo ya maeneobunge.

Kupitia afisa wa DPP Alex Akula, upande wa mashtaka umemomba hakimu mkuu Martha Mutuku kuondoa mashtaka hayo ila kesi itasalia kwa washtakiwa wenza wanne ambao sasa watajibu mashtaka upya.

Aidha Jumwa bado anakumbwa na mashtaka ya mauaji huku akitarajiwa kuhojiwa na bunge kabla ya kuapishwa rasmi kuwa waziri.