Waziri wa elimu nchini Eliud machogu, ameyatetea matokeo ya mtihani wa kitaifa wa kidato cha nne KCSE yaliyotolewa juma lililopita, akisema kuwa matokeo hayo hayatoi ishara kuwa uchaguzi huu ulishuhudia udanganyifu wa viwango vikubwa.

Akizungumza katika kikao na waandishi wa habari, Waziri Machogu ametete idadi ya alama za A zilizochapishwa katika mtihani wa mwaka jana, akieleza kuwa idadi ya wanafunzi waliopata alama ya A, ilikua ya chini ikilinganishwa na mwaka wa 2021.

Machogu amezitaja taarifa za zinazoeleza kuhusu udanganyifu kama propaganda, akiwataka wale walio na Ushahidi kuhusu na udanganyifu kuu kuuwasilisha

January 27, 2023