Maandamano ya Madaktari

Madaktari Kushiriki Maandamano ya Amani Jumanne kushinikiza Utekelezaji wa CBA

Muungano wa Madaktari nchini, KMPDU, umetangaza mipango ya kuandaa maandamano ya amani siku ya Jumanne ijayo, lengo likiwa ni kuendelea kuisukuma serikali kusikiliza kilio chao. Katibu Mkuu wa KMPDU, Davji Atellah, kupitia barua aliyoituma kwa Kamanda wa Polisi wa Kaunti ya Nairobi,…

Mgomo wa madaktari waingia siku ya 22 leo hii.

Muungano wa madaktari nchini KMPDU umeendelea kumkashifu waziri wa afya Susan Nakuhmicha kwa kupendekeza kupunguzwa kwa mishahara ya madaktari wanagenzi kinyume na ilivyoainishwa kwenye mkataba wa maelewano wa mwaka 2017. Wakiwahutubia waandishi wa habari jijini Nairobi,muungano huo umeeleza kuwa mshahara ambao wanagenzi…

Ghana - Kenya

Ghana Kuunga Mkono Azma ya Raila Odinga Kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika.

Serikali ya taifa la Ghana imeahidi kuunga mkono azma ya Kinara wa chama cha ODM Raila Odinga, ya kuwania wadhifa wa mwenyekiti wa Muungano wa Umoja wa Afrika (AU). Rais William Ruto, ambaye yupo katika ziara rasmi nchini Ghana, aliweka wazi taarifa…

Ajali - Salama Area

Watu 10 Waangamia Kwenye Ajali ya Magari 5 Kwenye Barabara ya Nairobi- Mombasa.

Watu kumi wamepoteza maisha yao huku wengine kumi na wawili wakijeruhiwa vibaya katika ajali mbaya ya barabarani iliyohusisha magari kadhaa, ikiwemo matatau na Trella, katika eneo la Salama kwenye barabara kuu ya Nairobi – Mombasa. Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa asasi…

Rev, John Kiplimo

Jimbo la Eldoret Lapata Askofu Mpya Msaidizi baada ya Uteuzi wa Papa Francis Leo

Jimbo Katoliki la Eldoret limepokea habari njema baada ya Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis, kumteua Padre John Kiplimo Lelei kuwa Askofu Msaidizi. Kabla ya uteuzi huu, Padre Lelei alikuwa akihudumu kama Vicar Generali wa Jimbo hilo la Eldoret. Taarifa rasmi…

Msajili mkuu mpya wa mahakama nchini Bi. Winfridah Mokaya

Msajili mkuu wa mahakama Winfridah Mokaya atwaa kiapo cha Utumishi.

Msajili Mkuu mpya wa Idara ya Mahakama Winfridah Boyani Mokaya ameapishwa hii leo na kutwaa wadhifa wake rasmi katika hafla iliyoandaliwa kwenye majengo ya mahakama ya upeo jijini Nairobi mchana wa leo. Hafla ya kuapishwa kwake ilihudhuriwa na maafisa mbalimbali wa mahakama…

Ajali ya Barabarani Narok

Naibu Kamanda wa Polisi wa Narok Afariki Katika Ajali ya Barabarani

Naibu Kamanda wa Polisi wa Narok, Calvins Ochieng Onganda, amefariki katika ajali ya barabarani iliyotokea mapema leo katika eneo la Ratili kwenye barabara kuu ya Narok – Bomet. Kulingana na ripoti ya Idara ya Usalama, ajali hiyo ilitokea wakati gari lake aina…

Watu 1,026 waaga dunia kufuatia ajali za barabarani mwaka huu.

Vifo vinavyotokana na ajali za barabarani vimeongezeka mwaka huu ikilinganishwa na mwaka jana. Kulingana na ripoti iliyotolewa na mamlaka ya uchukuzi na usalama barabarani NTSA, watu 1,026 wameaga dunia kati ya tarehe 1 mwezi januari na tarehe 20 mwezi machi kufuatia ajali…