Ajali ya Barabarani Narok

Naibu Kamanda wa Polisi wa Narok Afariki Katika Ajali ya Barabarani

Naibu Kamanda wa Polisi wa Narok, Calvins Ochieng Onganda, amefariki katika ajali ya barabarani iliyotokea mapema leo katika eneo la Ratili kwenye barabara kuu ya Narok – Bomet. Kulingana na ripoti ya Idara ya Usalama, ajali hiyo ilitokea wakati gari lake aina…

Watu 1,026 waaga dunia kufuatia ajali za barabarani mwaka huu.

Vifo vinavyotokana na ajali za barabarani vimeongezeka mwaka huu ikilinganishwa na mwaka jana. Kulingana na ripoti iliyotolewa na mamlaka ya uchukuzi na usalama barabarani NTSA, watu 1,026 wameaga dunia kati ya tarehe 1 mwezi januari na tarehe 20 mwezi machi kufuatia ajali…

Naibu Gavana Mteule wa Kisii Elijah Obebo

Gavana wa Kaunti ya Kisii Amteua Elijah Obebo Kuwa Naibu Wake Mpya

Gavana wa Kaunti ya Kisii Simba Arati amemteua Elijah Obebo kuwa naibu wake mpya, baada ya kubanduliwa kwa aliyekuwa naibu gavana, Robert Monda. Uteuzi huu umetangazwa kwa bunge la kaunti ya Kisii na Spika Philip Nyanumba katika vikao vya Jumatano. Spika Nyanumba…

AFisa wa zamani wa Magereza akamatwa Transmara

Afisa Mstaafu wa Magereza Atiwa Nguvuni kwa Njama ya Mauaji TransMara, Narok

Maafisa wa polisi katika eneo la TransMara, Kaunti ya Narok, wamefanikiwa kumkamata afisa mmoja wa zamani wa idara ya magereza, anayetuhumiwa kuhusika katika njama ya mauaji ya maafisa wawili wa idara hiyo kufuatia mzozo wa kifedha. Makachero wa idara ya DCI walifanikiwa…

Kenyatta

Masomo Yasitishwa katika Chuo Kikuu cha Kenyatta Kuwaomboleza Walioaga Dunia.

Usimamizi wa Chuo Kikuu cha Kenyatta umetangaza kusitisha shughuli za masomo katika chuo hicho kwa muda wa siku tatu, kufuatia ajali ya barabarani iliyosababisha vifo vya wanafunzi 11 jana jioni katika eneo la Voi. Notisi iliyochapishwa pia imeeleza kwamba mipango ya kuhamisha…

Mswada mpya wa nyumba za bei nafuu watiwa saini kuwa sheria.

Rais Ruto hii leo ametia saini Mswada mpya wa Nyumba za bei nafuu kuwa sheria katika ikulu ya Nairobi. Kutiwa saini kwa sheria hii kunamaanisha kuwa ushuru wa asilimia 1.5 kwa mapato ya wafanyakazi wote nchini umerejea. Itakumbukwa kuwa awali idara ya…

Maafisa wa Polisi washtakiwa kwa mauaji.

Maafisa 2 wa Polisi Wapatikana na Hatia ya Mauaji ya Mchungaji wa Ngamia, Tana River.

Mahakama kuu ya Garsen kutwa ya leo imewapata na hatia ya mauaji maafisa wawili wa polisi waliohusia katika mauaji ya mchungaji wa ngamia katika Kaunti ya Tana River miaka sita iliyopita. Katika uamuzi wake Jaji Stephen Githinji, amesema kwamba afisa Emmanuel Wanje…

Bei ya petroli, dizeli na mafuta taa yapungua kwa shilingi 7,5 na 4 mtawalia.

Wahudumu wa magari na bodaboda nchini wamepata afueni baada ya mamlaka ya kudhibiti kawi na petroli (EPRA) kutangaza punguzo la bei kwa bidhaa za petroli. Kulingana na taarifa iliyotolewa na mamlaka hiyo hii leo, bei ya Super Petrol itapungua kwa Ksh.7.21, Dizeli…