Radio Osotua › Local News

Mary Wanyonyi aapishwa rasmi kama mwenyekiti wa tume ya CRA

Local News July 17, 2023 Osotua

BY ISAYA BURUGU 17TH JULY 2023-Mary Wanyonyi ameapisha rasmi kama mwenyekiti mpya wa tume ya ugavi wa mapato nchini.

Jaji mkuu Martha Koome ameongoza hafla ya kuapishwa kwa Bi Wanyonyi anayekuwa mwenyekiti wa tatu wa tume hiyo.

Anachukua wadhifa huo kutoka kwa Jane Kiringai aliyestaafu mwezi Feburuari mwaka huu.

Rais  Ruto alimteua Bi  Wanyonyi kama mwenyekiti wa tume ya ugavi wa mapato  mnamo mwezi Mei mwaka huu wadhifa iliyokuwa ukigombaniwa  pia na  Thomas Ludindi Mwadeghu na Felicity Nkirote Biriri.