Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) imeibua wasiwasi kuhusu hali ya kisiasa ya sasa nchini, ikionya kwamba masuala kama vile uhuni na kutoaminiana yanaweza kudhoofisha uendeshaji wa uchaguzi ujao.
Wakizungumza wakati wa mkutano wa kifungua kinywa kati ya Muungano wa Sekta ya kibinafsi KEPSA na IEBC siku ya Jumatano, wadau waliashiria kuongezeka kwa hofu kuhusu vurugu za kisiasa sawa na kuongezeka kwa ushawishi wa pesa katika uchaguzi.
Vilevile waliashiria kile walichokielezea kama utamaduni wa uhuni ambapo wanasiasa wanadaiwa kuwatumia vijana kusababisha ghasia.
“We are prioritising legal reforms, we have engaged with Parliament and they are willing to help us fast track the changes in the laws that will enhance our capacity and ability to deliver transparent and credible elections,” Erastus Edung Ethekon, @IEBCKenya Chairperson pic.twitter.com/9LrHvih4dy
— KEPSA KENYA (@KEPSA_KENYA) April 15, 2026

