Ofisi ya msajili wa vyama vya kisiasa imekubali mabadiliko yaliyofanywa na chama cha jubilee ambapo katibu mkuu wa chama hicho Jeremiah kioni Pamoja na naibu mwenyekiti David Murathe waling’atuliwa mamlakani na viongozi wa chama hicho waliokutana na rais William Ruto.

Kupitia taarifa msajili wa vyama vya kisiasa Ann Nderitu ameeleza kuwa baraza la chama hicho lilibuniwa kwa njia inayofaa na hivyo lina uhuru wa kujitenga kama chama tanzu kwenye muungano wa azimio la umoja.

February 14, 2023