Radio Osotua › Local News

Rais William Ruto amteua Amin Ibrahim Mohammed kama mkurugenzi mpya wa idara ya DCI.

Local News October 15, 2022 Brigit Agwenge

Rais William Ruto amemteua Amin Ibrahim Mohammed kama mkurugenzi mpya wa idara ya DCI majuma matatu baada ya George Kinoti kujiuzulu kutoka kwa wadhfa huo.Mohammed alikuwa miongoni mwa watu watatu waliochaguliwa baada ya tume ya huduma kwa polisi NPS kuwahojiwa watu kumi siku ya jumanne.

Kabla ya uteuzi wake,Mohammed alikuwa akihudumu kama mkurugenzi wa idara ya masuala ya ndani katika tume ya NPS.