Radio Osotua › Local News

Siku ya maji duniani yaadhimishwa huku changamoto zikizidi kukumba sekta ya maji nchini

Local News March 22, 2023 Osotua

BY ISAYA BURUGU,22ND MARCH,2023-Kenya imeungana na ulimwengu hivi leo kuadhimisha siku ya upatikanaji wamaji ambayo huadhimisha kila tarehe 22 mwezi Machi kila mwaka.

Madhimisho haya yanandaliwa wakati sekta ya maji kote nchini inazidi kushudia changamoto mbali mbali zikiwemo, mabadiliko ya hali ya hewa ambayo yamesababaisha ukame,rasilimali haba za kifedha kuimarisha miundo msingi ya maji, na kukosa kumbatia teknologia.

Picha:Hisani

 

Kampuni za uzambazaji maji kote nchini zimejipata katika njia panda huku zikikumbwa na changamoto kadha wakadhaa katika mstakabali wa utekelezaji majukumu yao.Muhandisi Peter Kahotho ni mkurugenzi mkuu wa kampuni ya usambazaji maji ya Nyeri.

Kauli mbiyu yam waka huu ni kuharakisha mageuzi ili kusuluhisha tatizo la uhaba wa maji na viwango duni kwa usafi.