Raphael Tuju

    Waziri wa zamani wa Raphael Tuju hii leo alifika mbele ya Mahakama ya Kibera, ambapo alikana mashtaka ya kudaiwa kutoa taarifa za uongo.

    Tuju alifika mahakamani kufuatia wito uliotolewa na Hakimu Mkuu Mwandamizi Stella Atambo kwa ajili ya kujibu kesi inayohusiana na kutoweka kwake hivi karibuni, ambayo ilizua wasiwasi wa umma na kusababisha hatua za kisheria kutafuta ufafanuzi kuhusu mahali alipo.

    Kulingana na hati ya mashtaka, madai hayo yanahusiana na tukio la Machi 21, 2026.Waendesha mashtaka wanadai kwamba Tuju alimjulisha afisa wa polisi aliyehudumu katika Kituo cha Polisi cha Karen kwamba alikuwa anafuatiliwa na watu wasiojulikana na baadaye kutekwa nyara.

    Shitaka hilo liliposomwa mahakamani, Tuju alikana madai hayo na akakiri kutokuwa na hatia.

    Kupitia wakili wake, Tuju aliomba aachiliwe kwa dhamana, akibainisha kuwa kosa hilo limeainishwa kama kosa dogo na kuangazia rekodi yake ndefu ya utumishi wa umma.

    April 8, 2026