27TH DEC,2023- Afisa wa polisi aliye katika kituo cha polisi cha Ngusishi huko Buuri, Kaunti ya Meru hivi leo  alijipiga risasi na kujiua ndani ya nyumba yake katika boma la kituo hicho.

Koplo huyo, ambaye alikuwa msimamizi wa kituo cha polisi, alijipiga risasi mwendo wa saa 3 asubuhi na bunduki yake aina ya AK47, kulingana na ripoti ya polisi.

Ujumbe wa kujitoa uhai ulipatikana ukipendekeza masuala ya kifedha yanayohusisha uhusiano, iliongeza.

 

 

 

 

 

 

 

 

December 27, 2023