By Isaya Burugu ,Oct 15,2022-Rais  William Ruto amemteua  Amin Mohamed Ibrahim  kama mkurugenzi mkuu  wa idara ya upelelezi wa jinai nchini DCI.Uteuzi huo umechapishwa kwenye notisi katika gazeti rasmi la serikali ya hiyo jana.

Kabla ya uteuzi huo Ibrahim alikuwa akiongoza  kitengo cha maswala ya ndani na pia alikuwa amehudumu  kwenye nyadhifa mbali mbali  ikiwemo kuongoza kitengo cha uchunguzi   wa makosa ya jinai yaani CID  na kile cha uhalifu wa benki kati ya nyadhifa zingine kuu.

Tume ya  kitaifa ya huduma kwa  polisi  ilikuwa imewaorodhesha  watu 10 waliokuwa wametuma maombi ya kutaka wadhifa huo uliyowachwa wazi kufuatia kujiuzulu kwa George Kinoti kama mkurugenzi mkuu wa DCI .

Mnamo jumanne juma hili  kumi hao  walifika mbele ya jopo la mahiojiano  yaliyoendeshwa katika taasisi ya mafunzo ya serikali iliyoko Kabete kaunti ya Kiambu.

Wengine walioorodheshwa ni , Bernard Barasa Walumoli, Eliud Kipkoech Lagat, Gideon Nyale Munga, Esther Chepkosgei Seroney na  David Kipkosgey Birech.Wengine walikuwa Jonyo Michael Wiso, Nicholas Ireri Kamwende, Paul Jimmie Ndambuki na Dakta . Simon Mwangi Wanderi.

 

October 15, 2022