Gavana wa kaunti ya Narok Patrick Ntutu amezindua zoezi la ukaguzi wa orodha ya wafanyakazi wa serikali ya kaunti ya Narok, Pamoja na usajili wa kidijitali wa wafanyakazi wote kwenye kaunti hii.

Akizungumza ofisini mwake mapema leo, Gavana Ntutu amesema kwamba zoezi hili litasaidia serikali ya kaunti katika kupanga bajeti yake Pamoja na kuhakikisha kwamba wafanyakazi wasiotambulika wanaondolewa kwenye mfumo wa malipo na pia kuiwezesha kutambua maeneo ambayo serikali inahitaji kupunguza au kuongeza idadi ya wafanyakazi, na kuwakabili wafanyakazi hewa.

June 6, 2023