Rais William Ruto ameongoza hafla ya kuwapa bendera ya taifa na kuwatuma wanajeshi wa kenya katika taifa la Kidemokrasia la Congo, kusaidia taifa hilo katika vita dhidi ya kundi la waasi wa M23, kama mojawapo ya juhudi za Pamoja za mataifa ya afrika mashariki za kutuma kikosi cha kijeshi katika taifa hilo ili kurejesha amani.

Rais Ruto amesema kuwa taifa la Kenya limejitolea katika kushirikiana na mataifa ya ukanda wa Afrika mashariki ili kuinua ustawi wa ukanda huu hasa mataifa yanayokumbwa na misukosuko. Jeshi la kenya limeungana na wanajeshi kutoka mataifa jirani katika kikosi cha pamoja cha Majeshi ya ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EACRF) Kikosi hicho kinajumuisha wanajeshi kutoka Uganda, Sudan Kusini, Kenya na hata taifa la Rwanda.

Aidha rais pia aliwaombea wanajeshi hao baada ya kuwakabidhi rasmi bendera ya taifa kama njia ya kuwatuma rasmi katika shughuli hizo za kuweka amani, katika taifa hilo ambalo limekua katika hali ya misukosuko hasa kutokana na kero la waasi wa kundi la M23.

Share the love
November 2, 2022

2 Comments

  • F. Wekesa

    02/11/2022

    This is the only sweet thing Ruto has done since he took power. Guys, Congo is the “richest” country in Africa with over USD 1 trillion, equal to over Ksh. 150 trillion mineral resources which the UN are stealing away from the country and in turn supporting the M23 goons to destabilize the country while the UN mine and loot. When we win this war, I will officially move to DRC and make a home there in the land of Milk and honey. ☺

  • F. Wekesa

    02/11/2022

    And btw i foresaw this move amd even hoped that it will happen soonest when DRC asked to join the East African Community. Guys, with this country alone, East Africa will be the Luxembourg of Africa.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

%d bloggers like this: