BY ISAYA BURUGU TH AUG 2023-Mahakama imekataa kutoa ilani ya kusitisha utekelezwaji wa  sehemu za mswada wa bajeti  wa mwaka 2023 haswa  kusitoisha makato ya walioajiriwa na wajiri ili kufadhili muradi wa serikali wa ujenzi wa nyumba .

Mahakama hiyo imesema kuwa itasikiza na kufanya uamuzi wake  kuhusu kesi iliyowasilishwa na seneta wa Busia Okiya Omutahtah na wengine na kisha itafanya uamuzi kuhusu kesi za pingamizi kuhusu utekelezaji wa mswada huo wa bajeti kati ya tarehe 13 na tarehe 14 mwezi uajo wa Septemba.

Omutata na LSK na wengine waliowasilisha pingamizi hizo wakiwazomea majaji watatu wanaosikiliza kesi hizo  na kuwalaumu kwa kile walichokitaja kuwa kuegemea upande wa Serikali. Majaji wanaosikiliza kesi ni David Majanja, Jaji Christine Meoli na Jaji Lawrence Mugambi,

.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

August 7, 2023