Rais William Ruto ametoa mwito wa kumaliza ukabila na kudumisha umoja wa kitaifa, wakati wa hotuba yake katika hafla ya kuapishwa kwa Naibu Mkuu mpya wa Jeshi la Ulinzi la Kenya Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri na Makamanda wa Huduma katika Ikulu ya Nairobi.

Katika hotuba yake, Rais Ruto alisisitiza haja ya dharura ya kushughulikia ukabila akisema, “Ni matamanio yangu tuondoe ukabila, ubaguzi katika taifa letu.

Tuimarishe nchi yetu katika umoja, maendeleo, amani na utulivu.”Akitambua jukumu muhimu lililotekelezwa na Jeshi la Ulinzi la Kenya na sekta pana ya usalama, Rais Ruto alipongeza uzalendo na weledi wao.

Akiwa Amiri Jeshi Mkuu, Rais Ruto alihakikishia uongozi wa kijeshi msaada wake usioyumba na kujitolea kutoa mwongozo wa kimkakati.

March 9, 2024