Kenya Redcross
YouTube player

Wakaazi wa kijiji cha Kotel katika eneo la Naikarra Narok Magharibi, wamekua na tatizo la ugonjwa wa kimeta, kutokana na hulka ya ulaji wa nyama ya mifugo walio aga dunia. Wakaazi hawa hawakuwa na ufahamu wa athari za tabia hii na hivyo waliendelea na shughuli hii kwa muda hadi shirika la msalaba mwekundu lillipoamua kuingia kati na kujaribu kutatua tatizo hili.

Redcross
Jeremiah Sindi | Mhudumu wa afya wa Kujitolea (Community Health Volunteer) eneo la Naikarra, Narok Magharibi | Picha: John Waicua

Kupitia kwa wahudumu wa afya wa kujitolea waliopewa mafunzo maalum, maisha ya wanajamii hawa yameshuhudia mabadiliko ya kipekee huku sasa wakijiepusha zaidi na tabia ya ulaji wa nyama ya mifugo waliofariki. Pia wamekumbatia ujenzi na matumizi ya vyoo, jambo ambalo limewasaidia katika kuepuka magonjwa kama vile kipindupindu. Bw. Jeremiah Sindi ni mmoja wa wahudumu wa afya wa kujitolea katika jamii hii ambaye amekua akiwaelimisha wanakijiji jinsi ya kuishi maisha yasiyo na magonjwa, kwa kukumbatia maagizo na mwongozo wa maafisa wa afya.

Redcross
Bi. Nancy Musanga | Mhudumu wa afya wa Kujitolea (Community Health Volunteer) eneo la Naikarra, Narok Magharibi | Picha: John Waicua

Juhudi za wahudumu hawa wa kujitolea pia zimeleta mabadiliko katika kijiji cha Mashambani eneo hili la Naikarra, ambapo Bi. Nancy Musanga alijitwika jukumu la kuwafunza wanajamii jinsi ya kukabiliana na tatizo la kichaa cha Mbwa (Rabbies) ambalo limekuwa likiwakumba wanajijiji hawa kwa muda sasa. Bi Musanga ambaye alipata kuathiriwa na ugonjwa huu baada ya mifugo wake kuangamibaada ya kuambukizwa ugonjwa huu, anaeleza kuwa ujuzi ambao wanakijiji wamepokea umesaidia katka kukabiliana na athari za maambukizi ya ugonjwa huu. 

...Baadaye kidogo Ngombe wakawa ni kama wako na wazimu, wanaanza kupiga nyumba, wanapiga watu, wanataka kuwauma watu na ng'ombe wenzao...
Bi. Nancy Musanga
Mhudumu wa Afya wa Kujitolea
October 20, 2022