Naibu Rais Rigathi Gachagua amesema kuwa asilimia 70 ya mapato ya serikali hutumika kulipa deni la umma lililorithiwa kutoka kwa utawala uliopita.Gachagua kwa mara nyingine ameilaumu serikali iliyopita kwa changamoto za kiuchumi zinazoshuhudiwa nchini.

Akizungumza wakati wa Sherehe za Mahafali ya 92 ya KMTC katika uwanja wa Kasarani jijini Nairobi,naibu rais aliongeza kuwa Rais William Ruto alirithi deni la umma la Ksh.9.6 trilioni. Hata hivyo, alitoa wito wa tathmini ya ukweli, akisisitiza haja ya kufahamisha umma kuhusu hali mbaya ya awali ya uchumi wa Kenya.

December 7, 2023