Radio Osotua › Local News

Mamlaka ya Mawasiliano ya Kenya yatoa makataa ya siku 60 kwa kampuni za mwasiliano kuendelea kusajili laini za simu.

Local News October 17, 2022 Brigit Agwenge

Kampuni za mawasiliano kama vile Safaricom na Airtel  zimeagizwa kufunga laini za simu ambazo hazitasajiliwa katika siku 60 zijazo katika hatua ya kutekeleza uzingatiaji wa zoezi la usajili lililofungwa Jumamosi.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa Jumatatu, Mamlaka ya Mawasiliano ya Kenya (CA) imeruhusu dirisha la miezi miwili zaidi ili kuhakikisha kwamba zoezi la usajili linafuatwa kwa asilimia 100. Mwishoni mwa kipindi cha siku 60, mdhibiti wa sekta ya mwasiliano na teknolojia anatarajiwa kufanya ukaguzi ili kujua kiwango cha uzingatiaji.