Rais William Ruto ameongoza kongamano la ID4AFRIKA ambapo zoezi la kutengeneza vitambulisho vya kidigitali limezinduliwa.

Ruto ameeleza kuwa Kenya ni miongoni mataifa ya kwanza barani Afrika kuanzisha mfumo wa sera ya ulinzi wa data unaojumuisha sheria na kanuni za data ya kibinafsi.

Ruto pia amejvunia kuwa idadi ya huduma za serikali zinazopatikana kwenye mfumo wa kidijitali zimeongezeka kutoka 320 hadi 5,000 akifichua kuwa serikali inakusudia kufikia huduma zote 7000 kufikia mwisho wa mwaka huu ili kuwawezesha wananchi kupata huduma bila urasimu.

May 24, 2023