Radio Osotua › Local News

SERIKALI YA KAUNTI YA NAROK KUANZA KUWASAIDA WALIOATHIRIWA NA NJAA.

Local News October 11, 2022 John Waicua

Wakenya wapatao 240,000 katika kaunti ya Narok wanakumbwa na makali ya njaa baada ya kushuhudiwa kwa vipindi virefu vya jua na ukame unaokumba kaunti 23 kote nchini. Ni kutokana na hali hii ambapo viongozi wa serikali ya kaunti ya Narok wakiongozwa na gavana Patric Ole Ntutu pamoja na viongozi wa sekta mbalimbali katika kaunti ya Narok wameanzisha juhudi za kuwasaida wananchi kukabiliana na makali ya njaa. Gavana Ntutu pamoja na kamishena wa Narok Bw.Isaac Masinde wameongoza kikao cha kujadili mbinu mwafaka za kuwasaidia wananchi walio katika hatari zaidi.

This morning I held a meeting with the Narok County Commissioner at his offices. We are aware of the ongoing drought crisis in the country brought about by tough and changing climate conditions. Unfortunately, as a county, this challenge is with us. pic.twitter.com/u7aeMtfvZz

— Governor Patrick Ole Ntutu (@OleNtutuK) October 11, 2022

Akiwahutubia waandishi wa habari nje ya Ofisi yake kamishena Isaac Masinde amesema zaidi ya shule 130 katika kaunti ya Narok zinahitaji msaada wa chakula kutokana na makali ya njaa. Masinde amesema kuwa serikali kwa ushirikiano na mashirika yasiyo ya kiserikali wanafanya juhudi  za pamoja ili kuhakikisha kuwa wamesamabaza chakula cha msaada kwa maeneo yaliyoathirika. 

We are seized with the situation and at the moment we are laying down strategies to mitigate. As such, today’s meeting was to set the stage for critical intervention measures that we are deploying. pic.twitter.com/UOQpvTCSTF

— Governor Patrick Ole Ntutu (@OleNtutuK) October 11, 2022

Gavana Ntutukwa upande wake amesema kuwa sehemu zilizokabwa zaidi na njaa ni maeneo ya Mosiro Narok mashariki, Narosura, maji moto, eneo la Loita, Naikara, kapsasian eneo la Ilkeren Trasmara magharibi pamoja na eneobunge la Emurua Dikirr. Ntutu amesema serikali ya kaunti ya Narok itashirikiana na ile ya kitaifa kuhakikisha kuwa misaada mbali mbali imewafikia wakazi wa maeneo haya. 

Taarifa zaidi


SERIKALI YA KAUNTI YA NAROK KUANZA KUWASAIDA WALIOATHIRIWA NA NJAA.

Wakenya wapatao 240,000 katika kaunti ya Narok wanakumbwa na makali ya njaa baada ya kushuhudiwa kwa vipindi virefu…


Kenya yaungana na ulimwengu kusherehekea siku ya mtoto wa kike duniani.

Wenyeji wa kaunti ya Narok  wametakiwa kuhakikisha kuwa swala la ukeketaji linatokomezwa kikamilifu.Wito huu umetolewa huku Kenya ikiungana…


Kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka apinga uingizaji wa vyakula vya GMO humu nchini.

Kinara wa chama cha Wiper Kalonzo Musyoka amepinga vikali hatua ya kuondolewa kwa marufuku ya utengenezaji na uingizaji…