Wakenya wapatao 240,000 katika kaunti ya Narok wanakumbwa na makali ya njaa baada ya kushuhudiwa kwa vipindi virefu vya jua na ukame unaokumba kaunti 23 kote nchini. Ni kutokana na hali hii ambapo viongozi wa serikali ya kaunti ya Narok wakiongozwa na gavana Patric Ole Ntutu pamoja na viongozi wa sekta mbalimbali katika kaunti ya Narok wameanzisha juhudi za kuwasaida wananchi kukabiliana na makali ya njaa. Gavana Ntutu pamoja na kamishena wa Narok Bw.Isaac Masinde wameongoza kikao cha kujadili mbinu mwafaka za kuwasaidia wananchi walio katika hatari zaidi.

    Akiwahutubia waandishi wa habari nje ya Ofisi yake kamishena Isaac Masinde amesema zaidi ya shule 130 katika kaunti ya Narok zinahitaji msaada wa chakula kutokana na makali ya njaa. Masinde amesema kuwa serikali kwa ushirikiano na mashirika yasiyo ya kiserikali wanafanya juhudi  za pamoja ili kuhakikisha kuwa wamesamabaza chakula cha msaada kwa maeneo yaliyoathirika. 

    Gavana Ntutukwa upande wake amesema kuwa sehemu zilizokabwa zaidi na njaa ni maeneo ya Mosiro Narok mashariki, Narosura, maji moto, eneo la Loita, Naikara, kapsasian eneo la Ilkeren Trasmara magharibi pamoja na eneobunge la Emurua Dikirr. Ntutu amesema serikali ya kaunti ya Narok itashirikiana na ile ya kitaifa kuhakikisha kuwa misaada mbali mbali imewafikia wakazi wa maeneo haya. 

    Taarifa zaidi

    IEBC Yaibua Wasiwasi Kuhusu Hali Ya Kisiasa Nchini.

    Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) imeibua wasiwasi kuhusu hali ya kisiasa ya sasa nchini, ikionya kwamba…

    Zaidi Ya Lita Milioni 2.8 Za Pombe Haramu Zanaswa.

    Zaidi ya lita milioni 2.8 za pombe haramu zimekamatwa na zaidi ya washukiwa 900 wamekamatwa tangu Serikali ilipoanzisha…

    Opiyo Wandayi Asema Hakuna Sababu Ya Kujiuzulu.

    Waziri wa kawi Opiyo Wandayi amepuuza miito ya kujiuzulu kufuatia usafirishaji wa mafuta wa shilingi bilioni 4.8 nje…

    October 11, 2022