Wakenya wapatao 240,000 katika kaunti ya Narok wanakumbwa na makali ya njaa baada ya kushuhudiwa kwa vipindi virefu vya jua na ukame unaokumba kaunti 23 kote nchini. Ni kutokana na hali hii ambapo viongozi wa serikali ya kaunti ya Narok wakiongozwa na gavana Patric Ole Ntutu pamoja na viongozi wa sekta mbalimbali katika kaunti ya Narok wameanzisha juhudi za kuwasaida wananchi kukabiliana na makali ya njaa. Gavana Ntutu pamoja na kamishena wa Narok Bw.Isaac Masinde wameongoza kikao cha kujadili mbinu mwafaka za kuwasaidia wananchi walio katika hatari zaidi.

Akiwahutubia waandishi wa habari nje ya Ofisi yake kamishena Isaac Masinde amesema zaidi ya shule 130 katika kaunti ya Narok zinahitaji msaada wa chakula kutokana na makali ya njaa. Masinde amesema kuwa serikali kwa ushirikiano na mashirika yasiyo ya kiserikali wanafanya juhudi  za pamoja ili kuhakikisha kuwa wamesamabaza chakula cha msaada kwa maeneo yaliyoathirika. 

Gavana Ntutukwa upande wake amesema kuwa sehemu zilizokabwa zaidi na njaa ni maeneo ya Mosiro Narok mashariki, Narosura, maji moto, eneo la Loita, Naikara, kapsasian eneo la Ilkeren Trasmara magharibi pamoja na eneobunge la Emurua Dikirr. Ntutu amesema serikali ya kaunti ya Narok itashirikiana na ile ya kitaifa kuhakikisha kuwa misaada mbali mbali imewafikia wakazi wa maeneo haya. 

Taarifa zaidi

Douglas Kanja ateuliwa rasmi kutwaa wadhfa wa Inspekta jenerali wa polisi.

Douglas Kanja ambaye amekuwa akihudumu kama kaimu Inspekta jenerali wa polisi kwa majuma mawili, sasa ameteuliwa rasmi kutwaa…

Maafisa 8 Kugombea Nyadhifa za Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi wa Kitaifa na wa Utawala.

Tume ya Kitaifa ya Huduma ya Polisi (NPSC) imechapisha majina nane ya maafisa walio na nia ya kutwaa…

Polisi Wapiga Marufuku Maandamano Katikati Mwa Jiji la Nairobi.

Idara ya Polisi nchini imetangaza kupiga marufuku shughuli za maandamano katikati mwa jiji la Nairobi. Kaimu Inspekta Generali…

October 11, 2022