Wakenya wapatao 240,000 katika kaunti ya Narok wanakumbwa na makali ya njaa baada ya kushuhudiwa kwa vipindi virefu vya jua na ukame unaokumba kaunti 23 kote nchini. Ni kutokana na hali hii ambapo viongozi wa serikali ya kaunti ya Narok wakiongozwa na gavana Patric Ole Ntutu pamoja na viongozi wa sekta mbalimbali katika kaunti ya Narok wameanzisha juhudi za kuwasaida wananchi kukabiliana na makali ya njaa. Gavana Ntutu pamoja na kamishena wa Narok Bw.Isaac Masinde wameongoza kikao cha kujadili mbinu mwafaka za kuwasaidia wananchi walio katika hatari zaidi.

Akiwahutubia waandishi wa habari nje ya Ofisi yake kamishena Isaac Masinde amesema zaidi ya shule 130 katika kaunti ya Narok zinahitaji msaada wa chakula kutokana na makali ya njaa. Masinde amesema kuwa serikali kwa ushirikiano na mashirika yasiyo ya kiserikali wanafanya juhudi  za pamoja ili kuhakikisha kuwa wamesamabaza chakula cha msaada kwa maeneo yaliyoathirika. 

Gavana Ntutukwa upande wake amesema kuwa sehemu zilizokabwa zaidi na njaa ni maeneo ya Mosiro Narok mashariki, Narosura, maji moto, eneo la Loita, Naikara, kapsasian eneo la Ilkeren Trasmara magharibi pamoja na eneobunge la Emurua Dikirr. Ntutu amesema serikali ya kaunti ya Narok itashirikiana na ile ya kitaifa kuhakikisha kuwa misaada mbali mbali imewafikia wakazi wa maeneo haya. 

Taarifa zaidi

Maafisa wa Kliniki Wasitisha Mgomo baada ya Makubaliano na Wizara ya Afya

Muungano wa Maafisa wa Kliniki Nchini (KUCO) umesitisha mgomo wake wa kitaifa na kuwaagiza wanachama wake kurejea kazini…

Ndindi Nyoro abanduliwa kama mwenyekiti wa kamati ya Bajeti bungeni.

Mbunge wa Alego Usonga, Samuel Atandi amechaguliwa kuwa mwenyekiti mpya wa Kamati ya Bunge ya Bajeti na Matumizi…

Wakenya 1,356 Kuwania Nafasi za Mwenyekiti na Makamishna wa IEBC

Wakenya 1,356 wameorodheshwa kuwania nafasi za Mwenyekiti na Makamishna wa Tume Huru ya Uchaguzi na uratibu wa Mipaka…

October 11, 2022